Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 45 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 578 2025-06-12

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani kuimarisha uhifadhi wa mazingira ya Mradi wa Bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere ili kuhakikisha uendelevu wa Mradi huo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, katika kuimarisha uhifadhi wa mazingira ikiwemo uhifadhi wa Mazingira ya Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuendelea kupanda na kutunza miti kwenye vyanzo vya maji, kuendelea kutoa elimu ya mazingira, kusimamia utekelezaji wa Mwongozo wa Taifa wa Matumizi endelevu ya Ardhi Eneo la Hifadhi ya Mita 60 kutoka kwenye vyanzo vya maji, pamoja na kuunda kamati za mazingira kwa ajili ya kudhibiti uharibifu wa mazingira kwenye vyanzo vya maji.