Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 45 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 577 2025-06-12

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE K.n.y. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati mkubwa Soko la Mbagala Kizuiani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Halmashauri ya Manispaa ya Temeke imetenga shilingi milioni 800 kwa ajili ya kufanya ukarabati mkubwa wa masoko yake likiwemo soko la Mbagala Kizuiani.

Mheshimiwa Spika, usanifu na upembuzi yakinifu wa mahitaji ya ukarabati wa soko la Mbagala Kizuiani umeshakamilika na utekelezaji wake utaanza mapema katika mwaka wa fedha 2025/2026.