Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 45 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 431 2025-06-12

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -

Je, mafunzo gani yanatolewa na Serikali kwa Wanawake kuhusu usimamizi wa biashara za uchukuzi na mbinu bora za usafirishaji?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Tanzania kupitia Wizara mbalimbali na taasisi zake imeendelea kutoa mafunzo kwa wanawake wajasiliamali kuhusu biashara za uchukuzi na mbinu bora za usafirishaji. Mafunzo haya yanatolewa kwa lengo la kuwezesha wanawake kushiriki kikamilifu katika sekta ya uchukuzi ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikitawaliwa na wanaume.

Mheshimiwa Naibu Spika, mafunzo ya ujasiliamali yameendelea kutolewa kupitia taasisi zifuatazo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Small Industries and Development Organization (SIDO), Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) na National Economic Empowerment Council (NEEC, ambapo wanawake hupewa elimu ya namna ya kuanzisha, kuendesha, kukuza biashara za uchukuzi kama usafirishaji wa abiria, mizigo na usambazaji wa bidhaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, mafunzo haya ya udereva wa magari ya biashara yameendelea kutolewa kupitia taasisi zifuatazo: National Institute of Transport (NIT) na Vocational Education and Training Authority (VETA) ambapo wanawake wameendelea kufundishwa kuendesha magari makubwa (mabasi, malori, magari ya abiria, magari ya mizigo) pamoja na usalama barabarani.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia, hivi karibuni LATRA kupitia Vyuo vya NIT na CBE, wameanzisha mafunzo ya wahudumu wa mabasi ambao wengi wao ni wanawake. (Makofi)