Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 33 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 430 | 2025-05-27 |
Name
Ussi Salum Pondeza
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chumbuni
Primary Question
MHE. KILUMBE S. NG'ENDA K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu kwa wananchi hususan Wafugaji wanaolisha mifugo maeneo ya hifadhi ya reli? (Makofi)
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Reli Tanzania (TRC) limeandaa mpango maalum wa kuhakikisha masuala ya mazingira na jamii yanatekelezwa kwa kuzingatia sheria za Kitaifa na Kimataifa. Aidha, TRC imeendelea kutoa elimu kwa wadau mbalimbali wakiwemo wafugaji kupitia mpango maalum wa ushirikishwaji wa wadau yaani “Stakeholders Engagement Plan”.
Mheshimiwa Naibu Spika, elimu hii inatolewa katika shughuli za mradi za kila siku na kupitia kampeni maalum zinazofanyika kila baada ya miezi mitatu kwa lengo la kuhakikisha kunakuwepo usalama wa miundombinu ya reli kwa wadau.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ulinzi ni jukumu la kila mwananchi. Hivyo naomba kutumia fursa hii kuwaomba Waheshimiwa Wabunge kuungana Serikali na TRC katika kutoa elimu ya usalama wa miundombinu ikiwemo ya reli kwa wananchi wa maeneo yao.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved