Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 33 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 429 2025-05-27

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: -

Je, Serikali imefikia wapi katika utekelezaji wa Azimio la Bunge kuhusu ushirikiano kati ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na Manispaa – Moshi Mjini?

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Zimamoto na Uokoaji imepanga kukutana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Wizara ya Maji na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa ajili ya masuala ambayo yatawezesha utekelezaji wa Azimio la Bunge kuhusu ushirikiano baina ya Manispaa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika shughuli za uokoaji nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linaendelea na ushirikiano baina yake na Manispaa katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa magari ya zimamoto na uokoaji, kupanga miji, upitishaji wa michoro ya ujenzi, usimikaji wa fire hydrants na upatikanaji wa viwanja vya ujenzi wa vituo vya zimamoto na uokoaji nchini ikiwemo Manispaa ya Moshi Mjini, ahsante.