Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 33 Industries and Trade Wizara ya Viwanda na Biashara 425 2025-05-27

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU aliuliza: -

Je, Serikali imefanya tathmini gani ya vinywaji ilivyoruhusu kama pombe kuona kama havina athari kwa wananchi hasa vijana?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Viwango Tanzania (TBS) hufanya udhibiti wa bidhaa za pombe kwa kupitia mifumo iliyowekwa ili kuhakikisha ubora na usalama wake. Mifumo ya udhibiti inahusisha uandaaji wa viwango; uthibitishaji ubora wa pombe zinazozalishwa nchini na zinazotoka nje ya nchi; ukaguzi, uchunguzi wa kimaabara; ufuatiliaji katika soko; na kutoa mafunzo na elimu kwa wadau.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hufanya Tathmini kupitia ufuatiliaji wa bidhaa za pombe na imekuwa ikifanyika mara kwa mara ili kuendelea kubaini na kusimamia ubora wake.