Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 33 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 423 | 2025-05-27 |
Name
Maimuna Salum Mtanda
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Newala Vijijini
Primary Question
MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na upungufu wa watumishi hususan Walimu na Watoa Huduma za Afya - Newala Vijijini?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali iliidhinisha kibali na kuajiri Walimu 12,015 na watoa huduma za afya 13,625. Kati ya nafasi hizo walimu 30 na Watoa Huduma za Afya nafasi 42 waliajiriwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala ili kukabiliana na upungufu wa watumishi katika sekta hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kukabiliana na upungufu huo ambapo katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali imepanga kuajiri jumla ya walimu 10,652 na watoa huduma za afya 10,449 ambapo kati ya nafasi hizo, walimu wapya 49 na watoa huduma za afya nafasi 52 watapangiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Newala.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved