Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 33 | Public Service Management | Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) | 422 | 2025-05-22 |
Name
Nicodemas Henry Maganga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbogwe
Primary Question
MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa ajira kwa wahitimu wa vyuo nchini?
Name
Deus Clement Sangu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imetoa nafasi 47,404 za ajira mpya kwa kada mbalimbali ambazo utekelezaji wake unaendelea kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma na mamlaka nyingine na wasailiwa kutoka vyuo mbalimbali waliofaulu wameweza wamepangiwa vituo vya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali inatarajia kutoa ajira mpya 45,000 kwa kada mbalimbali ambazo utekelezaji wake utafanyika kabla ya mwaka huu wa fedha kwisha. Aidha, katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali imeidhinisha jumla ya nafasi 41,500 za ajira mpya kwa kada mbalimbali ili kuweza kuajiri wahitimu stahiki. Ninashukuru.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved