Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 420 2025-05-27

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO K.n.y. MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:-

Je, lini Vituo vya Afya Kitaya na Majengo - Nanyamba vitapatiwa magari ya kubeba wagonjwa?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya na Nanyumbu mwaka 2023/2024 imepokea magari mawili ya kubebea wagonjwa ambayo yamepelekwa kwenye Kituo vya Afya Majengo na Hospitali ya Mji wa Nanyamba. Aidha, Kituo cha Afya Kitaya kinahudumiwa na gari kutoka Hospitali ya Mji Nanyamba, ambapo umbali kati ya vituo hivyo ni takribani kilometa 50.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa kwa awamu kwa ajili ya vituo vya afya vyenye uhitaji kote nchini kikiwemo Kituo cha Afya Kitaya.