Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 419 2025-05-27

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Primary Question

MHE. DKT. MEDARD M. KALEMANI aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa vituo vya afya Kata za Nyamilembe, Kasenga na Ilyamachele vilivyoanza kujengwa kwa nguvu za Wananchi?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2024/2025, Serikali imetoa shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje OPD katika Kituo cha Afya Kasenga.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya Kata ya Nyamilembe kipo kwenye Mpango wa kupokea fedha kutoka Mfuko wa TASAF katika mwaka 2024/2025, ambapo tayari Halmashauri ya Wilaya ya Chato imewasilisha maombi makao makuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vituo vya afya vilivyoanza ujenzi kwa nguvu za wananchi katika Kata za Kimkakati kote nchini zikiwemo Kata za Nyamilembe, Kasenga na Ilyamchele katika Halmashauri ya Chato.