Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 33 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 417 | 2025-05-27 |
Name
Salim Mussa Omar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Gando
Primary Question
MHE. SALIM MUSSA OMAR aliuliza: -
Je, Serikali haioni haja ya kutengeneza Kanuni zitakazoweka kima cha chini cha mishahara ya Wafanyakazi wa Majumbani?
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Salim Mussa Omar, Mbunge wa Gando kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa wafanyakazi wa nyumbani na hivyo imeendelea kuweka kanuni tajwa mwaka 2022. Kupitia Tangazo la Kima cha Chini cha Mshahara Na. 687, Serikali iliweka kima cha chini cha mshahara kwa sekta binafsi ikiwemo sekta ya wafanyakazi wa nyumbani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa sheria, tangazo hili linadumu kwa miaka mitatu, na hivyo kwa sasa Serikali kupitia Bodi ya Kima cha Chini cha Mshahara kwa Sekta Binafsi inaendelea kukamilisha utafiti wa kima kipya cha chini cha mshahara ambacho pia kitajumuisha sekta ya wafanyakazi wa nyumbani. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved