Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 29 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 377 2025-05-21

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. FESTO R. SANGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itafikia makubaliano na kampuni zinazotoa huduma ya Internet kwa Satellite duniani kutoa huduma hapa nchini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kutoa huduma ya intaneti hapa nchini kwa kutumia satellite, kampuni inahitaji kuwa na leseni ya kutoa huduma hiyo kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Hadi sasa, TCRA imetoa leseni kwa mtoa huduma mmoja wa satellite (Connect Broadband Tanzania Limited) ambaye alipewa leseni mwaka 2021 baada ya kukikidhi vigezo vyote vinavyohitajika kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, maombi ya watoa huduma wote yamekuwa yanashughulikiwa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni, na pindi yanapokidhi vigezo wanapewa leseni. Aidha, utaratibu mzima wa upatikanaji wa leseni, aina ya leseni pamoja na masharti ya leseni vyote hivyo vinapatikana katika tovuti (website) ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Mheshimiwa Naibu Spika, TCRA inakaribisha na inaendelea kupokea maombi kutoka kwa Kampuni mbalimbali zenye sifa ya kutoa huduma za satellite kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zinazosimamia sekta ya mawasiliano hapa Nchini.