Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 29 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 375 | 2025-05-21 |
Name
Constantine John Kanyasu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Geita Mjini
Primary Question
MHE. HUSSEIN N. AMAR K.n.y. MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -
Je, Serikali haioni haja ya kukifufua Kiwanda cha Pamba na Mafuta Kasamwa kwa kuwa hivi karibuni nchi ilikabiliwa na uhaba wa mafuta?
Name
Exaud Silaoneka Kigahe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kaskazini
Answer
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Serikali kupitia Bodi ya Pamba (TCB) mwaka 2020 ilifanya tathmini juu ya hali ya viwanda vya kuchambua pamba nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, tathmini hiyo iliwezesha Chama cha Ushirika Geita kufanya maamuzi ya kufufua Kiwanda cha Kuchambua Pamba cha Kasamwa kupitia mkutano wa tarehe 27 Machi, 2025 kwa kukopa fedha katika Benki ya Azania, mkopo wa kiasi cha shilingi bilioni 8.68. Aidha, chama kimepanga kuanza na kiwanda cha kuchambua pamba na kiwanda cha kukamua mafuta kitafuata baada ya hapo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved