Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 29 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 373 2025-05-21

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -

Je, kwa nini Kampuni za CCECC na YAPI MARKEZI zinazojenga SGR Bukene zinatoa ajira zisizohitaji ujuzi kwa Vijana wanaotoka nje ya Bukene? (Makofi)

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Reli (TRC) inaendela na ujenzi wa Reli ya Kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza (Km 1,219), Tabora – Kigoma (Km 506) na Uvinza – Msongati (Km 282) ambao ni chachu katika uchumi wa Taifa. Utekelezaji wa mradi huu umetoa fursa za ajira kwa wenye ujuzi (skilled) na wasio na ujuzi (unskilled).

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ajira za wasio na ujuzi, mradi huu umetoa kipaumbele kwa wazawa katika maeneo ambayo yamepitiwa na mradi kwa kupewa ajira hizo kwa lengo la kuongeza ushiriki wa wananchi katika uchumi (local content).

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kumtoa hofu Mheshimiwa Selemani Zedi, Mbunge wa Bukene kuwa Serikali imekuwa ikizingatia ajira kwa wazawa ambao wamepitiwa na mradi katika maeneo yote ikiwemo Bukene.