Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 29 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 373 | 2025-05-21 |
Name
Selemani Jumanne Zedi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -
Je, kwa nini Kampuni za CCECC na YAPI MARKEZI zinazojenga SGR Bukene zinatoa ajira zisizohitaji ujuzi kwa Vijana wanaotoka nje ya Bukene? (Makofi)
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Reli (TRC) inaendela na ujenzi wa Reli ya Kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza (Km 1,219), Tabora – Kigoma (Km 506) na Uvinza – Msongati (Km 282) ambao ni chachu katika uchumi wa Taifa. Utekelezaji wa mradi huu umetoa fursa za ajira kwa wenye ujuzi (skilled) na wasio na ujuzi (unskilled).
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ajira za wasio na ujuzi, mradi huu umetoa kipaumbele kwa wazawa katika maeneo ambayo yamepitiwa na mradi kwa kupewa ajira hizo kwa lengo la kuongeza ushiriki wa wananchi katika uchumi (local content).
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kumtoa hofu Mheshimiwa Selemani Zedi, Mbunge wa Bukene kuwa Serikali imekuwa ikizingatia ajira kwa wazawa ambao wamepitiwa na mradi katika maeneo yote ikiwemo Bukene.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved