Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 29 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 372 | 2025-05-21 |
Name
Cecilia Daniel Paresso
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -
Je, lini Serikali italipa fidia na riba kwa wananchi wa Manyara Kibaoni Wilayani Karatu waliopisha upanuzi wa Uwanja wa Ndege Manyara?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali bado inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kulipa riba ya fidia kwa wakazi waliopisha upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Lake Manyara. Mara baada ya kupatikana fedha hizo, malipo ya riba kwa wananchi waliopisha upanuzi wa mradi huo yatafanyika. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved