Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 29 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 371 2025-05-21

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX K.n.y. MHE. SYLVIA F. SIGULA aliuliza: -

Je, lini Serikali itatokomeza uvuvi haramu katika Ziwa Tanganyika? (Makofi)

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO K.n.y. WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo TAMISEMI ili kuhakikisha rasilimali za uvuvi zinalindwa na kuvunwa kwa njia endelevu. Aidha, Wizara imeendelea kuimarisha vituo vyote vya ulinzi na usimamizi wa rasilimali za uvuvi vilivyopo katika ukanda wa Ziwa Tanganyika kwa kuvipatia vitendea kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hatua hiyo, Wizara imeendelea na mikakati ya matumizi ya teknolojia ya kisasa ya ndege nyuki katika kukabiliana na vitendo vya uvuvi haramu. Aidha, Wizara kwa kushirikiana na asasi zisizokuwa za kiserikali inaendelea kutoa elimu kwa jamii za wavuvi na wadau wengine juu ya athari za uvuvi haramu.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa wito kwa halmashauri kuendelea kushirikiana na Wizara katika kudhibiti vitendo vya uvuvi haramu. Pia, natoa wito kwa wavuvi wote nchini, wakiwemo wavuvi wa Ziwa Tanganyika kufanya shughuli zao kwa kuzingatia miongozo, taratibu, sheria na kanuni za uvuvi. Kwa kufanya hivyo tutakuwa tumetokomeza uvuvi haramu hapa nchini ikiwemo Ziwa Tanganyika.