Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 29 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 370 2025-05-21

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO K.n.y. MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE aliuliza: -

Je, nini mawanda ya Mradi wa Bonde la Mto Ngono lililofanyiwa upembuzi yakinifu ili liweze kuendelezwa na lini ujenzi wa Mradi huo utaanza?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Bonde la Mto Ngono ni miongoni mwa mabonde 22 ya kimkakati ambayo yamefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji. Bonde hili linajumuisha maeneo ya umwagiliaji ya Wilaya za Bukoba, Misenyi na Muleba, zikiwemo Skimu za Kyabaramba, Katoro, Ngarama, Kyakakera, Kabaijuga, Kaibanja, Kishege, Minazi, Buterankuzi (Bukoba), Nkenge, kafunjo, Butulage, Buchurago, Bulembo Kusini (Misenyi), Ikondo, Buyaga, Buhangaza, Muhutwe, Katoke, Kagoma na Kikuku (Muleba). Aidha, eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji katika bonde hili ni zaidi ya hekta 16,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na mchakato wa manunuzi kwa ajili ya kupata wakandarasi wa ujenzi wa skimu katika bonde hili unaendelea. Ujenzi wa skimu za Mto Ngono unatarajiwa kuanza mwaka huu wa fedha baada ya hatua za manunuzi kukamilika.