Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 29 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 369 | 2025-05-21 |
Name
Ally Anyigulile Jumbe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kyela
Primary Question
MHE. ALLY A. J. M. JUMBE aliuliza: -
Je, lini Miradi ya Maji katika Wilaya ya Kyela itakamilika?
Name
Kundo Andrea Mathew
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bariadi Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2024/25, Serikali imekamilisha utekelezaji wa Mradi wa Maji Lema, ambapo unanufaisha wananchi 3,357 waishio kwenye Kijiji cha Lema, kilichopo Wilayani Kyela, Mkoa wa Mbeya. Vilevile, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Miradi Minne ya Ngana, Sinyanga, Kyela - Kasumulu na Ipinda, wilayani humo, ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Miradi hiyo inatarajiwa kukamilika mwezi Disemba, 2025 na kunufaisha zaidi ya wananchi 110,000 waishio kwenye maeneo ya vijiji na Mitaa ya Wilayani Kyela.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved