Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 29 Water and Irrigation Wizara ya Maji 368 2025-05-21

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha mfumo wa maji taka Kiwanda cha A - Z ili kuondoa changamoto ya Wananchi wa Kata ya Olmot – Arusha?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Uondoshaji Majitaka wa Olmoti utakaonufaisha Kiwanda cha A to Z pamoja na wakazi zaidi ya 1,200 wa Kata ya Olmot – Arusha. Kazi zinazotekelezwa katika mradi huo ni pamoja na ulazaji wa mabomba umbali wa kilometa 9.206, ujenzi wa nguzo 15 za kushikilia bomba kwenye vivuko pamoja na ujenzi wa Chemba 188 za ukaguzi wa mfumo wa majitaka. Hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 78% na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2025.