Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 367 2025-05-21

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka walimu wa kike katika shule ambazo hazina walimu wa kike Wilayani Chemba?

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ina shule za msingi 113 na shule za sekondari 29. Aidha, shule zisizo na walimu wanawake ni shule za msingi 11 na shule za sekondari zote zina walimu wanawake.

Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo Februari na Machi, 2025, Serikali imeajiri walimu 15,925 ambapo Halmashauri ya Chemba imepokea walimu 93 wa (awali na msingi 40 na sekondari 53) wakiwemo walimu 32 wanawake na walimu 61 wanaume. Shule tatu za msingi ambazo ni miongoni mwa shule ambazo hazikuwa na walimu wanawake zimepangiwa walimu hao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuajiri walimu, wakiwemo walimu wanawake, kadiri ya upatikanaji wa fedha.