Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 29 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 366 | 2025-05-21 |
Name
Omari Mohamed Kigua
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilindi
Primary Question
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: -
Je, lini Serikali itajenga daraja linalounganisha Kijiji cha Negero – Kilindi?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa daraja linalounganisha Kijiji cha Negero – Kilindi katika kuchochea shughuli za kiuchumi katika eneo hilo. Katika mwaka 2023/2024, Serikali ilitumia shilingi milioni 70 kufanya usanifu wa Daraja la Mto Negero ili kupata gharama halisi za ujenzi wa daraja hilo. Usanifu ulikamilika mwezi Machi, 2025.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi inayoendelea sasa ni kupitia taarifa ya usanifu na baada ya kukamilika na kupata gharama halisi, daraja hili litaombewa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa wananchi wa eneo hilo wanatumia kivuko cha chuma cha waenda kwa miguu (Pedestrian Suspension Bridge) chenye upana wa mita 100 kilichojengwa na kukamilika Desemba, 2021 kwa gharama ya shilingi milioni 66.68 ili kuwapunguzia adha katika eneo hilo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved