Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 365 2025-05-21

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha maboma yaliyojengwa na Wananchi katika Mkoa wa Songwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2023/2024, Serikali imepeleka jumla ya shilingi bilioni 156.5 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya elimu na zahanati kote nchini ambapo kwa kipindi hicho, jumla ya shilingi bilioni 4.68 zimetumika kukamilisha maboma 51 ya zahanati na maboma 211 ya elimu katika Mkoa wa Songwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali imetenga shilingi bilioni 9.54 kwa ajili ya kukamilisha maboma ya madarasa 734 ya shule za sekondari na msingi, matundu 114 ya vyoo, nyumba za walimu sita na bweni moja. Aidha, Serikali imetenga shilingi bilioni 30.38 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma ya zahanati 346 kote nchini, ambapo Mkoa wa Songwe umetengewa shilingi milioni 752.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali imetenga shilingi bilioni 2.9 kwa ajili ya kukamilisha maboma ya madarasa 209 ya shule za sekondari na msingi, matundu 66 ya vyoo, mabweni mawili na maabara 12 za shule za sekondari katika Mkoa wa Songwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi kote nchini.