Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 46 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 596 | 2025-06-16 |
Name
Cecilia Daniel Paresso
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza: -
Je, Serikali imejipangaje kutatua changamoto zilizojitokeza wakati wa ununuzi wa mbegu za ruzuku kwa wakulima nchini?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, usambazaji wa mbegu za mahindi kwa mpango wa ruzuku ulianza msimu wa 2024/2025. Katika utekelezaji wa mpango huo, Serikali imebaini changamoto mbalimbali ikiwemo wakulima kukosa namba ya usajili ya ruzuku; bei elekezi ya ruzuku kushindwa kutekelezwa kwa wauzaji wadogo walioko katika ngazi za kata na vijiji; baadhi ya mawakala na makampuni ya mbegu wasio waaminifu kuuza mbegu nje ya mfumo wa ruzuku; na idadi ndogo ya wauzaji wa mbegu hususan katika ngazi za kata na vijiji.
Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kuchukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na changamoto hizo kwa ajili ya msimu wa 2025/2026. Hatua hizo ni kuhakikisha wakulima wa zao la mahindi wanasajiliwa kwa wakati katika mfumo wa pembejeo za kilimo; kutoa elimu kwa umma kuhusu utekelezaji wa mpango wa ruzuku ya mbegu za mahindi; kufanya mapitio ya bei elekezi ya mbegu inayotumika ili kuwezesha mawakala wadogo kuingizwa kwenye mfumo wa ruzuku; kuchukua hatua kali kwa mawakala wa mbegu watakaouza mbegu za mahindi bila kufuata bei elekezi ya ruzuku; na kuzielekeza Kampuni za mbegu kuongeza idadi ya mawakala wa mbegu wanaosambaza mbegu za ruzuku hususan vijijini.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved