Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 46 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 594 | 2025-06-16 |
Name
Katani Ahmadi Katani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tandahimba
Primary Question
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA K.n.y. MHE. KATANI A. KATANI aliuliza:-
Je, lini Serikali itawalipa Wakandarasi wa Miradi ya Maji fedha zao kutokana na miradi mingi kutokamilika kwa kukosa malipo kwa wakati?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kulipa madeni ya wakandarasi, wataalam washauri na watoa huduma mbalimbali wanaotekeleza au kutoa huduma kwenye ujenzi wa miradi ya maji nchini ikiwemo Wilaya ya Tandahimba. Hadi kufikia mwezi Mei, 2025, jumla ya shilingi 2,548,920,536.19 kati ya shilingi 3,999,970,936.19 za madai ya wakandarasi na watoa huduma wanaotekeleza miradi mbalimbali ya maji Wilayani Tandahimba zimelipwa.
Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali itaendelea kulipa madai yote ya wakandarasi, wataalam washauri na watoa huduma wa miradi ya maji nchini kadri fedha zinavyopatikana ili miradi hiyo iweze kukamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma iliyokusudiwa kwa wananchi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved