Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 46 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 593 2025-06-16

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

Je, lini Geti la kuingilia Watalii Hifadhi ya Mto Ugala Wilaya ya Urambo litawekwa?

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugala inakuwa miongoni mwa Hifadhi bora nchini, Serikali imepanga kuiendeleza Hifadhi hiyo kwa awamu ambapo katika awamu ya kwanza Serikali imetumia shilingi 2,000,000,000.00 kuboresha miundombinu muhimu ya Hifadhi ikiwemo ujenzi wa mtandao wa barabara hifadhini, ujenzi wa jengo la utawala, nyumba za watumishi, vituo vya askari, visima vya maji na maeneo ya kupumzika wageni.

Mheshimiwa Spika, mara baada ya kukamilika kwa awamu hii, Serikali itajielekeza kwenye kujenga malango manne ambayo ni Lunyeta, Lumbe, Iluma na Izengabatogilwe kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha.