Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 46 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 592 | 2025-06-16 |
Name
Janeth Elias Mahawanga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -
Je, Serikali ina Sera za kuwawezesha wanawake wajasiriamali kutumia teknolojia ya habari kuongeza ufanisi wa biashara zao?
Name
Dr. Selemani Said Jafo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisarawe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCHAL P. KATAMBI) K.n.y. WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia mamlaka zake ina sera mbalimbali za kuwawezesha wananchi wakiwemo wajasiliamali wanawake kutumia teknolojia ya habari ili kuongeza ufanisi wa shughuli zao ikiwemo biashara. Sera hizo ni pamoja na Sera ya Taifa ya Biashara ya Mwaka 2003 Toleo la 2023, Sera ya Taifa ya Posta ya Mwaka 2003, Sera ya Taifa ya Mawasiliano ya Mwaka 1997 na Sera ya Taifa ya TEHAMA ya Mwaka 2016 ambazo zinatambua Biashara Mtandao inayowezeshwa na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.
Mheshimiwa Spika, aidha, kwa kutambua uwepo wa changamoto za Teknolojia ya Habari katika kufanya biashara, Serikali imeandaa Mkakati wa Kitaifa wa Biashara Mtandao (National Electronic Commerce Strategy) ili kuwawezesha wajasiriamali wakiwemo wanawake kufanya biashara mtandaoni. Ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved