Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 46 | Finance | Wizara ya Fedha | 591 | 2025-06-16 |
Name
Mohammed Said Issa
Sex
Male
Party
ACT
Constituent
Konde
Primary Question
MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza: -
Je, changamoto zipi zinazorotesha ukusanyaji wa mapato katika mfumo mpya wa kuchakata Kodi ya Forodha ambao ni "single window"?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ahsante sana, single window ni dirisha moja la kufanikisha uwasilishaji wa nyaraka mbalimbali kutoka kwa wadau wote muhimu katika mnyororo wa ugomboaji mizigo ya forodha.
Mheshimiwa Spika, itakumbukwa kuwa kabla ya Mfumo wa Single Window, mteja alilazimika kuwasilisha nyaraka na vielelezo mbalimbali kwenda kila idara ya Serikali inayohusika katika mnyororo wa ugomboaji wa mizigo, na hivyo kusababisha usumbufu mkubwa na kuchelewesha ugomboaji wa mizigo forodhani.
Mheshimiwa Spika, ninapenda kutoa hofu kuwa single window haitaweza kupelekea uzoroteshaji wa ukusanyaji mapato ya Serikali bali utasaidia kuondoa usumbufu kwa wateja na kurahisisha ukokotoaji wa kodi mbalimbali kupitia Mfumo wa TANCIS uliohuishwa.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved