Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 46 | Finance | Wizara ya Fedha | 590 | 2025-06-16 |
Name
Michael Mwita Kembaki
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tarime Mjini
Primary Question
MHE. JANEJELLY J. NTATE K.n.y. MHE. MICHAEL M. KEMBAKI aliuliza: -
Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua masharti kandamizi kwa wawekezaji wa ndani kama kukadiria na kulipa kodi kabla ya kuanza biashara?
Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Bunge lako Tukufu, ilifanya Marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi (Tax Administration Act, 2015) Kifungu cha 22, ili kuahirisha wajibu wa kulipa kodi ya awamu chini ya Sheria ya Kodi ya Mapato kwa kipindi cha miezi sita tangu tarehe ambayo Nambari ya Utambulisho ya Mlipaji (TIN) ilipotolewa kwa mtu yeyote anayesajiliwa na kupewa TIN kwa mara ya kwanza.
Mheshimiwa Spika, kwa mabadiliko haya, mfanyabiashara aliyesajiliwa kwa mara kwanza atalipa jumla ya kodi aliyoahirishiwa baada ya miezi sita kwa awamu tatu. Lengo la mabadiliko haya ya sheria ni kuweka mazingira wezeshi kwa wafanyabiashara na wawekezaji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved