Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 25 | Works and Transport | Wizara ya Uchukuzi | 327 | 2025-05-15 |
Name
Margaret Simwanza Sitta
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Urambo
Primary Question
MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -
Je, lini Uwanja wa Ndege Urambo utawekwa uzio ili kuimarisha usalama?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali inakubaliana na pendekezo la ujenzi wa uzio ili kuimarisha usalama katika Kiwanja cha Ndege Urambo na tayari suala hili limejumuishwa katika rasimu ya Mpango Mkakati wa TAA wa miaka mitano ijayo.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwepo kwa mpango huo, TAA inaendelea na utekelezaji wa maagizo ya Kitaifa kuhusiana na ulinzi na usalama, ikiwemo ushirikishwaji wa wananchi kulinda mipaka kupitia uhamasishaji wa ulinzi shirikishi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved