Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 25 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 327 2025-05-15

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

Je, lini Uwanja wa Ndege Urambo utawekwa uzio ili kuimarisha usalama?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inakubaliana na pendekezo la ujenzi wa uzio ili kuimarisha usalama katika Kiwanja cha Ndege Urambo na tayari suala hili limejumuishwa katika rasimu ya Mpango Mkakati wa TAA wa miaka mitano ijayo.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwepo kwa mpango huo, TAA inaendelea na utekelezaji wa maagizo ya Kitaifa kuhusiana na ulinzi na usalama, ikiwemo ushirikishwaji wa wananchi kulinda mipaka kupitia uhamasishaji wa ulinzi shirikishi.