Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 1961-1995 | Session 1 | Sitting 1 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 323 | 2025-05-15 |
Name
Mwanaisha Ng'anzi Ulenge
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -
Je, upi mkakati wa kuwaandaa Wanawake wakulima wa mbogamboga Mkoani Tanga kwenye mpango wa Tanga kuwa hub ya kilimo cha mbogamboga?
Name
Hussein Mohamed Bashe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nzega Mjini
Answer
WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa engineer Mwanaisha Ulenge, kama ifuatavyo: -
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imekiwezesha Kituo cha Utafiti cha Mlingano TARI kuwa kituo mahiri katika uzalishaji wa mazao ya viungo, karafuu na mboga. Pia Wizara inaendelea kutoa mafunzo ya kanuni na teknolojia bora za kilimo cha mboga kushirikiana na sekta binafsi ikiwemo TAHA kujenga vituo na miundombinu ya kuhifadhi mazao ya mbogamboga ikiwemo vyumba vya baridi na kutoa mafunzo ya ukusanyaji, ufungashaji na uhifadhi wa mazao kabla ya kusafirishwa katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved