Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 1961-1995 | Session 1 | Sitting 1 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 322 | 2025-05-15 |
Name
Dr. Christina Christopher Mnzava
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: -
Je, nini mpango wa Serikali wa kuboresha makazi ya Askari Polisi Manispaa ya Shinyanga kwa kuwa ni duni sana?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Spika, ahsante. Serikali inatambua uchakavu wa nyumba za makazi ya askari polisi katika manispaa ya Shinyanga na mikoa yote kwa ujumla hapa nchini. Katika Manispaa ya Shinyanga zipo jumla ya nyumba 84 za makazi ya askari polisi ambazo ni chakavu. Tathmini ya uchakavu kwa ajili ya kuzifanyia ukarabati nyumba hizo imeshafanyika na kiasi cha fedha shilingi 1,848,000,000 kinahitajika.
Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutenga fedha toka kwenye Bajeti yake kila mwaka wa fedha ili kuweza kukarabati nyumba za makazi ya askari polisi hapa nchini zikiwemo za Manispaa ya shinyanga. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved