Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 25 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 320 | 2025-05-15 |
Name
Emmanuel Adamson Mwakasaka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tabora Mjini
Primary Question
MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza: -
Je, upi mkakakati wa Serikali kukarabati barabara za pembezoni Tabora Mjini?
Name
Zainab Athuman Katimba
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA): alijibu: -
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/2024, shilingi milioni 585.2 zilitumika kukarabati barabara zenye urefu wa kilomita 46.6, ujenzi wa kalavati 4 za box, ujenzi wa kalavati 10 za mduara, ukarabati wa daraja moja na ujenzi wa mitaro mita 500 za urefu katika kata za Ikomwa, Ifucha, Itetemia, Uyui, Misha, Itonjanda na Ndevelwa.
Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka 2024/2025, zimetengwa shilingi milioni 703.7 ambapo kazi za kukarabati barabara zenye urefu wa kilomita 61, ujenzi wa kalavati 2 za box, ujenzi wa kalavati 20 za mduara katika kata za Uyui, Tumbi, Kabila, Ikomwa, Ifucha, Ntalikwa, Itonjanda na Ndevelwa zimekwishaanza kufanyika na zinatarajiwa kukamilika ifikapo Julai 2025.
Mheshimiwa Spika, serikali itaendelea kuihudumia miundombinu ya barabara na madaraja zikiwemo barabara za pembezoni mwa Mji wa Tabora kwa kuzijenga, kuzikarabati na kuzifanyia matengenezo kulingana na upatikanaji wa fedha.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved