Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 46 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 586 | 2025-06-16 |
Name
Selemani Jumanne Zedi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -
Je, lini Zahanati za Buhulyu, Mogwa, Mwanzilwo na Gulyambi - Bukene zitaanza kutoa huduma?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kujenga vituo vya kutolea huduma na kuvisajili ili vianze kutoa huduma za afya. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2024/2025 jumla ya zahanati 1,158 zimejengwa na kusajiliwa na zinatoa huduma.
Mheshimiwa Spika, Zahanati ya Buhulyu, Mogwa na Gulyambi zimekamilika, zimesajiliwa na zinatoa huduma. Aidha, Zahanati ya Mwanzwilo ujenzi umefikia hatua ya ukamilishaji 80% ambapo Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Nzega imetenga shilingi milioni 30 katika mwaka wa fedha 2025/2026 kwa ajili ya ukamilishaji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved