Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 546 | 2025-06-09 |
Name
Emmanuel Lekishon Shangai
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Primary Question
MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. EMMANUEL L. SHANGAI aliuliza:-
Je, lini ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Wasso hadi Loliondo kilomita 10 utaanza?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Wasso hadi Loliondo yenye urefu wa kilomita 10 ni sehemu ya Barabara ya kutoka Mto wa Mbu hadi Loliondo yenye urefu wa kilometa 217. Serikali tayari imeanza taratibu za ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii kwa kuanza na sehemu ya Wasso hadi Loliondo yenye urefu wa kilometa 10 ambapo mkataba wa ujenzi umesainiwa tarehe 5 Juni, 2025 na taratibu za kuanza kazi za ujenzi zinaendelea. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved