Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 544 | 2025-06-09 |
Name
Issa Jumanne Mtemvu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kibamba
Primary Question
MHE. DOROTHY G. KILAVE K.n.y. MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:-
Je, lini Serikai itakamilisha ujenzi wa barabara kutokea Makondeko – Kwembe hadi Mloganzila?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TANROADS imekuwa ikijenga barabara ya Makondeko – Kwembe – Mloganzila yenye urefu wa kilometa 17.26 kwa awamu, ambapo kilometa 4.89 zimejengwa kwa kiwango cha lami kuanzia Mloganzila – Kibamba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2024/2025 Serikali kupitia TANROADS imepanga kuendelea na ujenzi wa barabara hii kwa urefu wa kilometa 1.7. Kwa sasa mradi upo kwenye hatua za manunuzi ya kumpata mkandarasi atakayetekeleza kazi za ujenzi, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved