Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 543 | 2025-06-09 |
Name
Zuberi Mohamedi Kuchauka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Liwale
Primary Question
MHE FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka huduma ya bure ya mtandao kwenye vyuo na shule zote nchini?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, UCSAF imefanikiwa kufikisha internet katika maeneo sita ya umma kikiwemo Chuo cha Maendeleo ya Jamii cha Rungemba (Mafinga), eneo la Bustani ya Nyerere Square (Dodoma), Ndaki ya Habari na Elimu Angavu (Chuo Kikuu cha Dodoma), Soko la Tabora, Kiembe Samaki (Unguja) na Soko la Buhongwa (Mwanza) na maeneo mengine 17 katika viwanja vya maonyesho ya Saba Saba. Lengo la Mradi huu ni kuongeza wigo na matumizi ya mawasiliano ya internet ya kasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile UCSAF imekuwa ikitekeleza mradi wa kuzipatia shule za Serikali vifaa vya TEHAMA ili kuziunganisha na mtandao wa internet, ambapo mpaka sasa takribani shule 1121 zimenufaika kupitia mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa miradi hii ya kufikisha huduma ya internet katika maeneo ya vyuo na katika shule za Serikali unaendelea kadiri ya upatikanaji wa fedha kwa lengo ya kuzifikia shule zote na maeneo yote yenye uhitaji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved