Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 542 | 2025-06-09 |
Name
Saashisha Elinikyo Mafuwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Hai
Primary Question
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:-
Je, Serikali haioni ipo haja ya kupitia upya mikataba ya mashamba ya ushirika na kufanya tathmini ya ardhi ya mashamba hayo?
Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Answer
NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wizara ya Kilimo kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika inafanya mapitio na tathmini ya mikataba ya uwekezaji katika mashamba ya ushirika. Baadhi ya mikataba inayoendelea kufanyiwa mapitio ni ya mashamba ya Vyama vya Ushirika vya Miradi ya pamoja ya Kyumasha, Murososangi, Fonrwa, Lyamungo Amcos, Manush Narumu; Mashamba ya Vyama vya Ushirika vya Kilimaboro, Masama Mula, Kibosho Kati na Chama Kikuu cha Ushirika Kilimanjaro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Tume ya Maendeleo ya Ushirika imeweka moduli ya uwekezaji kwenye Mfumo wa Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (MUVU) kwa lengo la kufanyiwa upembuzi na tathmini. Hadi sasa jumla ya mashamba 408 ya vyama vya ushirika yenye thamani ya shilingi bilioni 271.48 yameingizwa kwenye mfumo huo.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved