Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Industries and Trade | Wizara ya Viwanda na Biashara | 541 | 2025-06-09 |
Name
Abeid Ighondo Ramadhani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ilongero
Primary Question
MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: -
Je, Serikali ina mkakati gani wa kutoa elimu ya Mfumo wa Stakabadhi Ghalani kwa Wakulima ili kuondoa changamoto zilizopo - Singida Kaskazini?
Name
Dr. Selemani Said Jafo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kisarawe
Answer
WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Bodi ya Usimamizi wa Stakabadhi za Ghala (WRRB) na wadau wengine katika Mnyororo wa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ilibaini uwepo wa changamoto ya uelewa kuhusu mfumo unavyofanya kazi kwenye baadhi ya maeneo, hivyo kusababisha kuundwa kwa timu maalum, ili kutoa elimu katika Mikoa ya Singida, Manyara na Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu kuhusu Mfumo wa Stakabadhi za Ghala imetolewa na itaendelea kutolewa katika ngazi ya Halmashauri na Kata zote nchini zinazozalisha mazao mbalimbali, ikiwemo dengu na mbaazi katika Mkoa wa Singida, Jimbo la Singida Kaskazini katika Kata za Mwasauya na Msange.
Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la utoaji wa elimu kuhusu matumizi ya mfumo huo itakuwa endelevu, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved