Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 540 | 2025-06-09 |
Name
Suma Ikenda Fyandomo
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ORAN M. NJEZA K.n.y. MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza: -
Je, lini Serikali itawapa makoti ya kujikinga na baridi Askari Polisi wanaofanya kazi katika Mkoa wa Mbeya?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, makoti ya kujikinga na baridi ni miongoni mwa sare za Jeshi la Polisi, ambazo Askari wanaofanya kazi kwenye mikoa yenye hali ya hewa ya baridi kali hupatiwa. Mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa mikoa ambayo Askari Polisi wanapewa makoti ya kujikinga na baridi kali wakiwa kazini, kama sare ya Jeshi la Polisi. Mikoa mingine inayopewa makoti ya kujikinga na baridi ni Iringa, Njombe, Songwe, Rukwa, Arusha, Manyara, Kilimanjaro pamoja na Wilaya ya Lushoto katika Mkoa wa Tanga, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved