Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Lands, Housing and Human Settlement Development | Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi | 539 | 2025-06-09 |
Name
Josephine Johnson Genzabuke
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. KAVEJURU E. FELIX K.n.y. MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha zoezi la upimaji wa ardhi katika Halmashauri ya Kasulu DC?
Name
Geophrey Mizengo Pinda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kavuu
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Wizara ilitoa fedha kiasi cha shilingi milioni 50 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, kwa ajili ya kupanga, kupima na kumilikishwa viwanja 500 kupitia Programu ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi (KKK).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutumia fedha hizo, zaidi ya vipande vya ardhi 1,200 vilitambuliwa, viwanja 866 vimepimwa na kuidhinishwa katika Mitaa ya Nyangwa, Makere na Kalimungoma. Zoezi la kumilikisha viwanja 866 vilivyoidhinishwa linaendelea kupitia mazoezi ya Kliniki za Ardhi, Ofisi za Halmashauri na Ofisi ya Ardhi, Mkoa wa Kigoma, ambapo jumla ya Hatimilki 47 zimeandaliwa na kati ya hizo, 37 zimekabidhiwa kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na zoezi la utambuzi na upimaji ardhi, kazi ya kuhuisha mipaka baina ya Vijiji vya Kagerankanda na Uvinza vilivyopakana na Msitu wa Hifadhi wa Makere Kusini pamoja na Kitalu cha Uwindaji ilifanyika, na pia, ukaguzi na uidhinishaji wa upimaji wa vijiji hivyo viwili unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, eneo ambalo wananchi wa Kitongoji cha Katoto watahamishiwa kupisha eneo wanaloishi kwa sasa limetengwa, ikiwa ni utekelezaji wa uamuzi wa Baraza la Mawaziri kuhusu utatuzi wa migogoro katika vijiji/mitaa 975. Kadhalika, zoezi la urasimishaji makazi katika mitaa mbalimbali linaendelea, ambapo jumla ya viwanja 4,813 vimepimwa na kuidhinishwa katika Halmashauri ya Mji wa Kasulu.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved