Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 538 | 2025-06-09 |
Name
Francis Kumba Ndulane
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilwa Kaskazini
Primary Question
MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:-
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Wilaya ya Kilwa?
Name
Prof. Adolf Faustine Mkenda
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Rombo
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo cha Ufundi Stadi cha Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa Vyuo 64 vya VETA vinavyojengwa na Serikali katika Wilaya ambazo zilikuwa hazijajengewa Vyuo vya Ufundi Stadi pamoja na Chuo kimoja cha Mkoa wa Songwe ambao ulikuwa hauna Chuo cha VETA cha Mkoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya kwanza ya ujenzi wa Chuo cha VETA cha Wilaya ya Kilwa unatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.6 ambapo hadi sasa kiasi cha shilingi 682,881,780.24 kimetumika. Aidha, ujenzi wa Chuo hiki umefikia 40% na unatarajiwa kukamilika mwezi Novemba, 2025.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved