Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Rais TAMISEMI. | 535 | 2025-06-09 |
Name
Selemani Jumanne Zedi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukene
Primary Question
MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -
Je, lini Serikali itamaliza tatizo la upungufu wa Watumishi wa Kada ya Afya – Bukene?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kutoa vibali vya ajira kila mwaka, ambapo kuanzia mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2024/2025 jumla ya watumishi wa kada ya afya 34,720 wameajiriwa na kupangiwa vituo kote nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020/2021 hadi 2024/2025 Halmashauri ya Wilaya ya Nzega imepangiwa jumla ya watumishi 111, ambao wamepangwa katika Hospitali ya Wilaya, vituo vya afya na zahanati. Kati ya hao, Jimbo la Bukene limepelekewa jumla ya watumishi 59.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kuajiri watumishi wa sekta ya afya kwa awamu na kuwapanga katika maeneo yenye upungufu wa wataalam hao ikiwemo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nzega.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved