Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 42 | Youth, Disabled, Labor and Employment | Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu | 533 | 2025-06-09 |
Name
Minza Simon Mjika
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:-
Je, nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inawawezesha kiuchumi Watu wenye Ulemavu.
Name
Paschal Katambi Patrobas
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shinyanga Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Minza Simon Mjika, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuwawezesha kiuchumi Watu wenye Ulemavu, Serikali imeendelea kufanya yafuatayo: -
(1) Kutoa Mikopo ya 10% isiyokuwa na riba inayotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ambapo watu wote wenye ulemavu wametengewa asilimia mbili;
(2) Utekelezaji wa takwa la Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura 440 la kutenga 30% ya zabuni za umma kwa ajili ya wanawake, vijana, wazee na watu wenye Ulemavu;
(3) Utekelezaji wa mipango ya maendeleo endelevu ya watu wenye ulemavu na ile ya kibajeti ikiwemo fungu maalum kwa wenye ulemavu;
(4) Kuwapatia elimu itakayowawezesha kushiriki katika shughuli jumuishi za kiuchumi; na
(5) Utekelezaji wa miongozo mbalimbali ukiwemo ule wa matumizi ya teknolojia saidizi ili kuwawezesha nao kushiriki katika shughuli za kiuchumi.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved