Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 25 | Regional Administration and Local Government Authorities | Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji | 319 | 2025-05-15 |
Name
Shabani Omari Shekilindi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Lushoto
Primary Question
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza: -
Je, lini Serikali itapeleka Gari jipya la Wagonjwa Hospitali ya Wilaya ya Lushoto kwa kuwa lililopo limechakaa?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto mwaka 2023/2024 imepokea magari mawili ya kubebea wagonjwa na kupelekwa katika Vituo vya Afya vya Mlola na Mtae. Kwa sasa Hospitali ya Wilaya ya Lushoto inatumia gari la kubebea wagonjwa kutoka kwenye Kituo cha Afya Mlola wakati taratibu za matengezo ya gari la hospitali ya wilaya zikiendelea.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma za afya nchini; na Hospitali ya Wilaya ya Lushoto itapelekewa gari.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved