Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 19 Sitting 21 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 272 2025-05-09

Name

Abdi Hija Mkasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Micheweni

Primary Question

MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukiboresha Kituo cha TEHAMA kilichopo Wilaya ya Micheweni?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ilitekeleza mradi wa ujenzi wa vituo 11 vya TEHAMA, Unguja na Pemba ambapo kwa kila wilaya kimejengwa kituo kimoja kwa madhumuni ya kuwapa fursa wananchi wa Zanzibar kujifunza na kutumia TEHAMA kwa ajili ya manufaa yao wenyewe ili kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni. Kituo cha TEHAMA Sokoni kilichopo Wilaya ya Micheweni ni miongoni mwa vituo hivyo ambapo kinaendelea kutoa huduma kama ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali kuhusu kukiboresha kituo husika kilichopo katika Wilaya ya Micheweni, inaashiria kuwa ipo changamoto. Hivyo, Wizara kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi itafanya tathmini ili kujua mahitaji halisi ya kituo hicho kwa lengo la kufanya maboresho yanayohitajika. (Makofi)