Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 21 | Information, Communication and Information Technology | Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari | 272 | 2025-05-09 |
Name
Abdi Hija Mkasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Micheweni
Primary Question
MHE. ABDI HIJA MKASHA aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kukiboresha Kituo cha TEHAMA kilichopo Wilaya ya Micheweni?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) ilitekeleza mradi wa ujenzi wa vituo 11 vya TEHAMA, Unguja na Pemba ambapo kwa kila wilaya kimejengwa kituo kimoja kwa madhumuni ya kuwapa fursa wananchi wa Zanzibar kujifunza na kutumia TEHAMA kwa ajili ya manufaa yao wenyewe ili kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kiutamaduni. Kituo cha TEHAMA Sokoni kilichopo Wilaya ya Micheweni ni miongoni mwa vituo hivyo ambapo kinaendelea kutoa huduma kama ilivyokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali kuhusu kukiboresha kituo husika kilichopo katika Wilaya ya Micheweni, inaashiria kuwa ipo changamoto. Hivyo, Wizara kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi itafanya tathmini ili kujua mahitaji halisi ya kituo hicho kwa lengo la kufanya maboresho yanayohitajika. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved