Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 17 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia | 224 | 2025-05-05 |
Name
Dr. Medard Matogolo Kalemani
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Chato
Primary Question
MHE. DKT. MEDARD M. KALEMANI aliuliza:-
Je, lini Ujenzi wa Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam cha masuala ya samaki eneo la Kasagara - Chato ulioanza 2021 utakamilika?
Name
Omary Juma Kipanga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mafia
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam eneo la Kasagara – Chato ulipaswa kuanza mwaka 2021 na kukamilika mwezi Mei, 2023. Ujenzi huo haujakamilika kutokana na changamoto za mkandarasi kushindwa kuendelea na ujenzi kwa muda mrefu hivyo kupelekea Serikali kuanza mchakato wa kusitisha mkataba wa utekelezaji wake. Taratibu za kufunga mkataba huo kisheria zinaendelea na mara zitakapokamilika Serikali itaanza mchakato wa kumtafuta mkandarasi mwingine ili kuendelea na ujenzi. Ninakushukuru sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved