Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 17 | Information, Culture, Arts and Sports | Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo | 221 | 2025-05-05 |
Name
Nusrat Shaaban Hanje
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza:-
Je, Serikali inafanya maandalizi gani kuhakikisha nchi yetu inafanya vizuri katika Mashindano ya AFCON 2027?
Name
Hamis Mohamed Mwinjuma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muheza
Answer
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya michezo katika Majiji ya Dar es Salaam, Arusha, Dodoma na Visiwani Zanzibar, kwa ajili ya kufanikisha mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON, 2027) yanayotarajiwa kufanyika nchini kwa kushirikiana na Nchi za Kenya na Uganda. Aidha, kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tunasimamia malezi ya timu ya vijana kimkakati ili kuhakikisha tunakuwa na timu bora yenye viwango wa ushindani wa kimataifa. Baadhi ya masuala yaliyofanyika ni pamoja na kuanzisha programu za kuendeleza vipaji kwa kuzishirikisha timu za vijana waliochini ya miaka 17, waliochini ya miaka 23 na kutumia wachezaji wa diaspora.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango mingine ni kuboresha mikakati ya upatikanaji wa vifaa mbalimbali vya michezo, kuandaa benchi la ufundi lililo bora, kuandaa programu za lishe, kuandaa kambi za mazoezi ya muda mrefu, kuandaa michezo ya kirafiki ya kimataifa na kuboresha na kusimamia maslahi ya wachezaji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved