Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 17 | Information, Culture, Arts and Sports | Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo | 220 | 2025-05-05 |
Name
Ng'wasi Damas Kamani
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU K.n.y. MHE. NG’WASI D. KAMANI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti maudhui yasiyo na maadili katika mitandao ya kijamii kwa maslahi ya afya ya akili na watoto?
Name
Hamis Mohamed Mwinjuma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muheza
Answer
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeweka mikakati na inaendelea kuchukua hatua za kiudhibiti kuhusiana na maudhui yasiyo na maadili katika anga la mtandao hapa nchini, ikiwemo mitandao ya kijamii. Kufikia Tarehe 31 Machi, 2025 TCRA imeweza kubaini na kufungia tovuti, akaunti za mitandao ya kijamii, majukwaa, blogs na kadhalika, zipatazo 80,171 zilizokuwa zinachapisha maudhui yaliyo kinyume na maadili na yenye kuhatarisha afya ya akili na watoto. Zoezi hili ni endelevu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea kuendesha na kutoa mafunzo ya weledi kwa waandishi wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na wachapishaji wa maudhui mtandaoni. Mafunzo haya yanawajengea uwezo washiriki katika kutambua maudhui ghushi mitandaoni, uandaaji wa makala pamoja na ujenzi wa taswira ya nchi ili kuendelea kulinda utamaduni ulio salama kwa makuzi ya Jamii ya Watoto wa Kitanzania.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved