Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 17 | Energy and Minerals | Wizara ya Madini | 219 | 2025-05-05 |
Name
Sebastian Simon Kapufi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mpanda Mjini
Primary Question
MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:-
Je, Halmashauri ya Mpanda inanufaika vipi na mauzo ya mchanga wa marudio ya madini katika Kata ya Misunkomilo, Mpanda? (Makofi)
Name
Anthony Peter Mavunde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Dodoma mjini
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI K.n.y. WAZIRI WA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha kuanzia Julai, 2024 hadi Machi, 2025 jumla ya tani 2,498.16 za makinikia ya shaba (copper concentrates) zilichenjuliwa kutoka katika Kata ya Misunkomilo ambapo madini ya shaba yenye thamani ya shilingi bilioni 16.01 yalipatikana na Serikali kunufaika kwa kukusanya shilingi bilioni 1.12 kupitia mrabaha na ada ya ukaguzi. Aidha, jumla ya shilingi milioni 48.02 zilikusanywa, kama tozo ya huduma (service levy) ambapo, Halmashauri za Mpanda Mjini na Nsimbo zilinufaika. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved