Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 17 | Home Affairs | Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi | 218 | 2025-05-05 |
Name
Zahor Mohamed Haji
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mwera
Primary Question
MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza:-
Je, Serikali imejiandaaje kukabiliana na Biashara Haramu ya Usafirishaji wa Binadamu na Dawa za Kulevya kwani mbinu za uhalifu zimebadilika?
Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepo wa uhalifu wa usafirishaji haramu wa binadamu hapa nchini na kwamba, mbinu za utendekaji wake zimekuwa zikibadilika. Katika kupambana na biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu, Serikali ina mikakati mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuwa na Mpango Kazi wa Kitaifa wa Kuzuia na Kupambana na Usafirishaji Haramu wa Binadamu, kutoa mafunzo kwa wasimamizi wa Sheria na wadau mbalimbali, kuratibu kampeni ya kutoa elimu kwa umma kuhusu uhalifu huu na madhara yake, mpango wa kuanzisha Kituo cha Kupokelea Taarifa za Usafirishaji Haramu wa Binadamu na mpango wa kuanzisha Mfumo wa Kielektroniki wa Kukusanya, Kusimamia na Kuhifadhi Taarifa za Usafirishaji Haramu wa Binadamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kukubaliana na mabadiliko ya mara kwa mara ya mbinu za uhalifu wa dawa za kulevya, Serikali imekuwa ikiwajengea uwezo maafisa wa udhibiti kwa kuwapatia mafunzo, ushiriki wa mikutano na vikao vya kimkakati vya kubadilishana taarifa za uzoefu na nchi na taasisi mbalimbali za kimataifa katika udhibiti wa dawa za kulevya. Ahsante. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved